Habari

Muswada wa sheria ya ndoa kurudishwa kwa wananchi kutolewa maoni

Serikali imejiandaa kurudia kukusanya maoni ya wananchi ili kukamilisha muswada wa sheria ya ndoa ili kukamilisha kubadilika kwa sheria hiyo.

5

Kauli hiyo imetolewa Ijumaa hii bungeni mjini Dodoma, na waziri wa katiba na sheria, Dk Harrison Mwakyembe, akijibu swali lililouliza kuhusu kurejeshwa bungeni kwa muswada huo kwaajili ya kuufanyia marekebisho.

“Sheria ya ndoa ya mwaka 71 ni matokeo ya mjadala mpana na shirikishi kupitia walaka wa serikali namba moja wa mwaka 69. Lengo la mjadala huo lilikuwa ni kupata muafaka kuhusu maudhui ya sheria hiyo ambayo inagusa imani, mila na desturi za watanzania,” alisema Mwakyembe.

“Baada ya miaka zaidi ya 20 kupita tangu sheria hiyo ya ndoa itungwe, serikali kupitia tume ya kurekebisha sheria iliifanyia mapitio sheria hiyo na kubaini maeneo kadhaa yenye udhaifu na hivyo kuhitaji kufanyiwa marekebisho. Kutokana na maoni ya tume wizara ya mambo ya katiba na sheria iliandaa mwaka 2008 waraka wa baraza la mawaziri uliokuwa na mapendekezo ya marekebisho ya sheria ya ndoa ya mwaka 71,” alisisitiza.

“Kwa kuzingatia chimbuko la sheria hiyo, baraza liliiagiza wizara kuandaa waraka maalumu wa serikali ya white paper ili kupata mjadala mpana na shirikishi kama ilivyokuwa awali. Mapema mwaka 2010 wizara ilikamilisha maandalizi ya waraka huo kubainisha hoja za wananchi walizotakiwa kuzitolea maoni,” aliongeza.

“Serikali inalazimika kurudia taratibu za awali kususanya maoni ya wananchi na kufanyia marekebisho sheria ya ndoa na kwamba mchakato huo ulisitishwa kwa kuwa tume ya mabadiliko ya katiba ilikuwa ikikusanya maoni kuhusu mabadiliko ya katiba. Hivyo walidhani wananchi wangetoa pia maoni juu ya sheria hiyo lakini haikuwa hivyo. Zoezi la kukusanya maoni ya wananchi litakamilika muda si mrefu.”

BY: EMMY MWAIPOPO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents