Burudani

Muziki ni biashara, taarabu ikifanya vizuri naimba – Dogo Janja

Msanii wa muziki kutoka Tip Top Connection, Dogo Janja amedai yeye ni mfanyabiashara kwenye muziki hivyo anafanya muziki wowote ambao anaona unafanya vizuri sokoni kwa muda huo.

Dogo Janja

Rapa huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo Kidebe, amedai soko la muziki wa Bongo halihitaji msanii ambaye anafanya muziki wa aina moja kwa muda mrefu bila kubadilika.

“Najitahidi nifanye muziki mkubwa kuonyesha nimekuwa, muziki ninaofanya ni kama unaofanywa na King Kiki,” Dogo Janja alikiambia kipindi cha Ladha 3600 cha EFM. “Naboresha video zangu na kufanya kazi itakayoacha alama hata kama sipo. Mimi nimfanya biashara usishangae leo hii nikiambiwa taarabu inauza mimi nikafumua dude,

Rapa huyo amewataka mashabiki wa muziki wake kukaa mkao wa kula kwaajili ya ujio wake mpya ambapo amedai atakuwa tofauti kama watu walivyomzoea.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents