Mwanafunzi auwa wenzake 17 kwa kuwapiga risasi
Mwanafunzi mwenye miaka 19 nchini Marekani, Nikolaus Cruz amewaua wenzake 17 kwa kuwapiga risasi, shambulio hilo lilitokea Florida.
Mshambuliaji huyo ambaye alikuwa amebeba bunduki alianza kushambulia bila ya mpangilio nje ya shule hiyo kabla ya kushambulia ndani.
Kamanda wa polisi katika eneo hilo, amesema mshambuliaji huyo alifukuzwa shule kutokana na utovu wa nidhamu. Tayari polisi wamemkamata kijana huyo.
Shirika la Upelelezila Marekani FBI limesema linashirikiana na polisi, kufanyia uchunguzi tukio hilo.
Rais Donald Trump kupitia ukurasa wake wa twitter amewaondolea hofu raia wa Marekani, kwa kusema kuwa usalama upo kwa mtoto, mwalimu na mtu yeyote yule.
My prayers and condolences to the families of the victims of the terrible Florida shooting. No child, teacher or anyone else should ever feel unsafe in an American school.
— Donald J. Trump (@realDonaldTrump) February 14, 2018
Just spoke to Governor Rick Scott. We are working closely with law enforcement on the terrible Florida school shooting.
— Donald J. Trump (@realDonaldTrump) February 14, 2018