Mwanafunzi wa chuo Kikuu ajiua
Mwanafunzi wa chuo Kikuu cha Tumaini, huko maeneo ya Kurasini Sheila Wasukira (22), amekutwa amekufa chumbani kwa mpenzi wake baada ya kujinyonga kwa kutumia kitanzi cha kamba alichokitundika juu ya nondo kwenye dirisha la sebuleni.
Mwanafunzi wa chuo Kikuu cha Tumaini, huko maeneo ya Kurasini Sheila Wasukira (22), amekutwa amekufa chumbani kwa mpenzi wake baada ya kujinyonga kwa kutumia kitanzi cha kamba alichokitundika juu ya nondo kwenye dirisha la sebuleni.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke Kanda Maalum Dar es Salaam, Emmanuel Kandhihab amesema kuwa tukio hilo limetokea jana saa 12 asubuhi, Mbagala Sabasaba.
Amesema msichana huyo alikwenda kumtembelea rafiki yake Peter Luoga (35), anayeishi Kurasini ambapo asubuhi alikutwa akiwa amejinyonga na hakuacha ujumbe wowote. Maiti imehifadhiwa chumba cha maiti Hospitali ya Temeke na polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.
Polisi inaendelea kufanya uchunguzi kwa ajili ya kujua sababu za binti.