Burudani

Mwanamuziki nguli wa Kenya Achieng Abura afariki dunia

Mwanamuziki mkongwe wa nchini Kenya na aliyewahi kuwa Principal kwenye mashindano ya Tusker Project Fame, Achieng Abura amefariki dunia.

achieng-abura-celeb-chat-800x776

Kwa mujibu wa The Standard, amefariki Alhamis hii kwenye hospitali ya taifa ya Kenyatta jijini Nairobi. Bi. Abura alikuwa amelazwa katika wodi binafsi akitibiwa ugonjwa ambao haujajulikana.

Bi. Abura Alifariki dunia mida ya saa 12 jioni. Mapema mwezi huu, muimbaji huyo aliandika kuwa afya yake si nzuri na madaktari walimshauri aongeze uzito kisha kuupunguza kupitia mazoezi.

Chanzo cha karibu na familia yake kilidai kuwa alihamishwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi baada ya hali yake kuwa mbaya.

Wasanii mbalimbali wa Kenya wametuma salamu zao za rambirambi kupitia mitandao ya kijamii. Hawa ni baadhi yao.

Avril

My day ends on a sad note..don’t know what to say…RIP Achieng Abura :'( ..

Nameless

So sad to hear of your passing dear sister….Rest in peace Achieng Abura.

Akothee

You’ve done your part….it’s a journey…I mourn you ! RIP #RIPAchiengAbura

Sauti Sol

Our heartfelt condolences to the family and friends of the late Achieng Abura. She was a natural talent, mentor to us all. This is a big blow to the music industry! #Rip #RipAchiengAbura #Shujaa

The King Kaka

Rest In Peace.
Achieng Abura.
Safiri Salama, tutaonana Baadaye.

Amani

R.I.P. Achieng Abura ????…a lovely woman who was passionate about music #legend

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents