Mwanamuziki nguli wa Kenya, Benga Joseph Kamaru afariki dunia
Mwanamuziki nguli raia wa Kenya, Benga Joseph Kamaru amefariki dunia hapo jana siku ya Jumatano katika hospitali ya MP Shah (MP Shah hospital) alipokuwa akipatiwa matibabu.
Mzee Kamaru amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 79 huku akikumbukwa zaidi miaka ya 1980 kwa vibao vyake vingi mashuhuri vikiwemo ‘Tiga Kuhenia Igoti’ (Usihadae mahakama), na ‘Muhiki wa Mikosi’ alivyokuw akiimba kwa lugha ya Kikuyu.
Rais Uhuru Kenyatta na viongozi mbalimbali wa Kenya wameonyesha kuguswa na kifo chake na kuposti ujumbe mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter.
Benga legend musician Joseph Kamaru is dead. Kamaru passed on Wednesday evening while receiving treatment at the MP Shah hospital. He died at the age of 79 years. #NTVAtOne @KenMijungu pic.twitter.com/r8EtUGf6mk
— NTV Kenya (@ntvkenya) October 4, 2018
What a sad moment for the lovers of Benga! Waking up another day with a sad news that Kenya has lost a big icon in the music industry. He has enriched Kikuyu culture perfectly and in a big way. We'll live to remember Mzee Joseph Kamaru. Deepest condolences to family.#RIPKamaru pic.twitter.com/7T3qC33Kaj
— H.E President William Ruto (Commentary) (@WilliamsMkenya) October 4, 2018
Kamaru aliyezaliwa mwaka 1939 na kufariki dunia hapo jana Oktoba 3, 2018 anakadiriwa kuwa na nyimbo zaidi ya nyimbo 2000.