Habari

Mwandishi wa habari auwawa Mexico

Muandishi wa habari aliyekuwa akiandika na kuripoti habari za uchunguzi zinazohusu madawa ya kulevya na ulanguzi nchini Mexico ameuwawa.

Javier Valdez, aliyewahi kushinda tuzo mbali mbali za uandishi wa habari zake aliuwawa siku ya jana (Jumatatau) katika mji wa Culiaciana kaskazini mwa mji wa Sinaloa.

Watu waliokuwa na silaha walimshambulia muandishi huyo kwa kumpiga risasa alipokuwa ndani ya gari lake wakati akiwa anaeleka kazini. Mwandishi huyo aliyejikita katika kuandika habari hizo alikuwa akiandika huku akijua kuwa anataraisha maisha yake.

Kwa kipindi cha miezi miwili mpaka sasa waandishi wa habari wanne katika nchi hiyo wameuwawa. Kwa mujibu wa CPJ( Committee to Protect Journalists)waandishi wa habari 40 waliuwawa kutokana na kurepost habari za madawa nchini Mexico tangu mwaka 1992.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents