Mwanariadha aangua kilio baada ya kuwa mshindi wa nne michuano ya European (+video)
Mwanariadha wa Israeli, Lonah Salpeter amejikuta akimwaga machozi hadharani mara baada ya kushika nafasi ya nne kwenye michuano ya European mbio za mita 5,000.
https://www.youtube.com/watch?v=N92Yo8Ma_l8
Mashindano hayo yaliyofanyika Berlin mashabiki wameshuhudia mwana dada, Salpeter ambaye ni mzaliwa wa Kenya anayeiwakilisha Israeli akipoteza matumaini ya ushindi hata wanafasi ya pili mara baada ya kujisahau na kuanza kusherehekea kabla ya raundi ya mwisho haijafikia kikomo na hivyo kujikuta akiangukia kwenyenafasi ya nne.
Siku ya Jumatano ya wiki iliyopita Lonah Salpeter aliweza kushinda mbio za mita 10,00o kabla ya kuingia kwenye kinyang’anyiro hicho cha mita 50,000 na kujikuta akiambulia patupu kutokana na kuamini kuwa muda wa raundi hiyo umekamilika kumbe ulikuwa umebaki mzunguko mmoja.
Ngolo kante sister usilie nyamaza hayo ndo mashindano kuna kushinda na kushindwa