Burudani

Mwanaume mwenye mvuto zaidi duniani Michael B. Jordan, amtangaza mpenzi wake (+ Video)

Baada ya miezi kadhaa ya tetesi , sasa mchezaji filamu maarufu wa Marekani Michael B. Jordan amethibitisha kuwa na mahusiano na Lori Harvey.

Wawili hao wamezungumzia kuhusu mapenzi yao, kupitia kurasa zao rasmi za Instagram siku ya Jumapili, huku wakishirikisha umma picha za mapenzi yao katika ukurasa huo wa Instagram.

Jordan, ambaye amekuwa msiri kuhusu maisha yake ya mapenzi, alikuwa wa kwanza kushirikisha umma picha yao kwenye Instagram.

Lori Harvey ni mwanamitindo

Michael B. Jordan alitangazwa kama mwanaume mwenye muonekano mzuri zaidi duniani mwaka 2020.

Mchezaji filamu Michael Jordan B. mwenye umri wa miaka 33 alionekana katika picha moja ya snap na Harvey, kabla ya kuonesha akimbusu. Alimshirikisha Harvey picha hizo, pamoja na mpiga picha Leo Volcy.

Harvey – ambaye aliasiliwa na Steve Harvey baada ya kumuoa mama yake 2007 Marjorie Bridges – alishirikisha umma picha hizo akiwa na Michael Jordan B. dakika chache tu baadae.

Lori ni mwanamitindo na amekuwa akionesha mitindo ya Dolce and Gabbana, katika wiki za mitindo za Paris na Milan.

Watu maarufu akiwemo mcheza filamu Gabrielle Union na mwanamuziki wa rap Teyana Taylor, walituma jumbe zao kuonesha upendo wao kwa wapenzi wao.

https://www.instagram.com/tv/CJ8FhGUBTsq/

https://www.instagram.com/tv/CJ8FhGUBTsq/

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents