Michezo
Mwenyekiti wa FA Greg Dyke amesema hatogombea tena nafasi hiyo Mwezi june
Greg Dyke ni mwenyekiti wa chama cha soka cha England FA ameamua kujiengua kwenye wadhifa huo ifikapo mwezi june,mwaka huu baada ya muda wake kumalizika.
Kwa mujibu wake Dyke hatogombea tena nafasi hiyo,ambayo alichaguliwa mwaka 2013 na amekitumika chama cha soka kwa miaka mitatu.Na alikua na lengo la kuongeza mwaka mmoja zaidi.
Dyke wakati akichukua uongozi kutoka kwa David Bernstein,alisema England inapaswa fika nusu fainali ya Euro 2020, na kutwaa kombe la dunia mwaka 2022.
Lakini mwenyekiti huyu ametoa maelezo katika mkutano wa bodi ya chama cha FA ilipokutana katika uwanja wa Wembley na akaeleza ” kama mnavyofahamu mapema mwezi January nilitangaza nitaendelea kuwa mwenyekiti kwa mwaka mmoja zaidi ila nafikiri yale hayakua maamuzi sahihi.