Tragedy
Mwili wa Langa kuagwa mchana wa leo nyumbani kwao
Mwili wa rapper Langa Kileo aliyefariki dunia wiki iliyopita, unatarajiwa kuagwa leo nyumbani kwao Mikocheni, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa ratiba ya mazishi iliyotolewa, mwili wake ulidaiwa utawasili nyumbani asubuhi na heshima za mwisho kuanza kutolewa saa saba hadi saa nane. Baada ya hapo utapelekwa kwenda kuzikwa kwenye makaburi ya Kinondoni.