Mahojiano
Mzazi Willy: “Alikiba anapendwa sana Kenya, Ubunifu katika Kaka Tuchat ya Roma na Stamina sawa na Nitarejea ya Diamond” – Video
Mtangazaji wa Radio Citizen kutoka nchini Kenya 🇰🇪 na mkali wa kipindi cha #MamboMseto @mzaziwillytuva ameisifia sana ngoma ya @staminashorwebwenzi na @roma_zimbabwe #Kakatuchat akisifia sana ubunifu kwenye hiyo ngoma ukilonganisha na gharama waliyotumia.
Mbali na hilo @mzaziwillytuva amelimiminia sifa kundi la muziki kutoka Kenya @sautisol kwa kusema kuwa vijana wengi na wasanii wanatakiwa kujifunza kupitia kwao kutokana na aina ya muziki wanaofanya na hata jinsi wanavyoishi. Pia ameutaja wimbo wa @diamondplatnumz #Nitarejea kama wimbo bora kwake kutokana na ubunifu wake.