Mzee Kikwete ampongeza Mwana FA kwa kuingia kwenye ujasiriamali, awataka wasanii wengine wabadilike
Rais Mstaafu wa awamu ya 4 Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amempongeza msanii wa Bongo Fleva, Mwana FA kwa kuingiza sokoni bidhaa yake mpya ya Body Spray ‘FYTbyFALSAFA’ .
Mzee Kikwete kupitia ukurasa wake wa Twitter, ameeleza kuwa kipindi cha utawala wake, aliwashauri wasanii wa muziki hapa Tanzania kuwekeza nje ya muziki.
Kuna siku nilimsihi @MwanaFA na wanamuziki wengine kufanya shughuli nyingine zaidi ya muziki pekee. Nimefarijika leo kunitembelea na kutambulisha bidhaa yake mpya ya “body spray”. Hii ni hatua kubwa na nzuri kwa vijana wetu. Tuwaungishe! pic.twitter.com/zqpE4e6UGk
— Jakaya Kikwete (@jmkikwete) December 19, 2018
Body Spray hizo kwa mujibu wa Mwana FA mwenyewe, zitauzwa kwa Tsh elfu 4000 kwa bei ya reja reja na zitaanza kupatikana wiki ijayo.