Burudani
Mzee Yusuf kurejea jukwaani
Baada ya kupotea kwa muda wa mwezi mmoja, mfalme wa taarabu, Mzee yusuf kutoka kwenye kundi la Jahazi Modern Taarab sasa amepanga kurejea jukwaani kwa style mpya atakayoitabulisha Ijumaa ya tarehe kumi na mbili katika ukumbi wa Travertine Magomeni.
Msemaji wa bendi hiyo, Seif Magwaru, amesema kwamba, Mzee yusuf ambaye alifanyiwa upasuaji wa goti mwishoni mwa mwaka jana sasa amepata afueni na yuko tayari kabisa kukonga mioyo ya mashabiki wake. Bongo5 inamtakia Mzee Yusuf na Bendi yake kila la kheri