Burudani
Mzee Yusuph kumshirikisha Vanessa Mdee na Dully Sykes
Mzee Yusuph anajaribu kuingia kwenye soko la muziki wa Bongo Flava kwa kishindo.
Akiongea na Bongo5, Mzee Yusuph alisema anatarajia kuwashirikisha Vanessa Mdee na Dully Sykes. Amedai kuwa sio mara yake ya kwanza kufanya kazi na wasanii wa Bongo Flava.
“Kama unakumbuka nimefanya nyimbo na Chidi Benz, nimefanya na Off Side Trick, nimefanya na wasanii wengi wa muziki huo,” alisema.