Burudani
Mzee Yusuph kuongeza mke wa tatu?
Muimbaji wa muziki wa Taarab nchini ambaye pia ni mkurugenzi wa kundi la Jahazi Modern Taarabu, Mzee Yusuph huenda akaoa mke wa tatu hivi karibuni.
Mzee Yusuph akiwa na mke wake mkubwa Leila
Tayari muimbaji huyo ana wake wawili, Leila Rashid na Chiku ambao inasemekana wakiwa hawapatani hata kidogo kiasi cha kurushiana vijembe katika mitandao.
Mzee Yusuph amethibisha mpango huo kupita U Heard ya XXL, Clouds FM.
Amedai kuwa wivu ni jambo la kawaida na hashangai kuona wake zake wakipigana vijembe. Mzee Yusuph amesema kuongeza mke mwingine huenda ikawa dawa ya wake zake hao na kwamba hana mpango wa kuwapatanisha kwa kuwa hakuna hata mmoja aliyeonyesha chuki kwa mwenzake akiwa nao.
Mzee Yusuph akiwa na mke wake mdogo Chiku