Burudani
Mzee Zorro kumpa shavu Mwana F.A
Yule mkali wa muziki wa kizamani ambaye hadi sasa anakimbiza katika muziki wa Bongo fleva maarufu kama muziki wa kizazi kipya, Zihir Zorro anatarajia kufanya Remix ya wimbo wake uliotamba wa Fanya vitu vyako, akiwa na mr Blue na Baby Boy
kutoka Zizzu Fashion. amesema kwa sasa anataraji kuja kivingine kabisa katika Remix ya wimbo huo kwa kumuweka pale kati msanii mwana Fa, kwakuwa ameridhishwa sana na kazi zake. Amesema baada ya hapo anarajia baada ya wiki mbili hivi, aweze kuingia Location kwaajili ya kuirudia na video ya wimbo huo, ambayo kwa muonekano huo mpya atakuwepo Fa
Hapa mzee Zorro akiteta na mwanaye Banana Zoro, katika moja ya matamasha waliyofanya