Habari

Nabii wa nyoka aonekana Nigeria kwa TB Joshua

Nabii alisababisha utata nchini Afrika Kusini, mwaka 2015, baada ya kuwafanya waumini wake kula nyoka, panya na nywele ameonekana kwenye ibada nchini Nigeria ya muhubiri maalufu TB Joshua.


Penuel Mnguni

Muhubiri Penuel Mnguni ameoneaka katika ibada iliyoongozwa na mhubiri TB Joshua katika kanisa lake na aliweza kutoa ushuhuda umaosema kuwa ”nilianza kutizama TV za Emmanuel TV na kumsikiliza nabii TB Joshua, nikafahamu kuwa nilichokuwa nikifanya haikiendani na maandiko. Na nilivyofahamu kuwa lilikuwa shambulio nikaja hadi kwa TB Joshua ili anikomboe.”

Kupitia akaunti yake ya twitter Muhubiri Joshua aliweza kutwit kwa kuonesha kuwa alimpokea mchungaji huyo katika kanisa lake.

Nabii Mngui amebadilisha moyo wake, kwa mujibu wa gazeti la Citizen baada ya kujikuta akiandamwa mara kwa mara na kupelekea kushtakiwa na chama cha kupambana na dhuluma dhini ya wanyama (Society for the Prevention of Cruelty to Animals) Afrika Kusini, hata hivyo mastaka hayo yalifutwa mwaka 2015 Julai baada ya kukosekana ushahidi wa kutosha.

Na Laila Sued

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents