Burudani

Naitamani sana nafasi ya Urais – Kala Jeremiah

Msanii wa muziki wa hip hop, Kala Jeremiah amefunguka kwa kusema kuwa hawezi kugombea ubunge kwani tayari ameshafanya kazi hiyo kwa miaka mingi na sasa anasubiri muda ufike aweze kugombea nafasi ya Urais.

Akiongea na umati wa watu uliojitokeza katika show ya ‘Wapo Tour’ya rapa Nay wa Mitego iliyofanyika Dar Live weekend hii, Kala atiwata mashabiki wake wajiamini katika mambo yao kama yeye anavyoamini siku moja anawekuwa Rais.

“Urais ndiyo ishu kwa sasa, kusema ukweli tayari nimeshakuwa mbunge kwa miaka mingi hata mashabiki wangu wanajua. Lakini kusema tena niende kugombea ubunge hapana siwezikufanya hivyo kwa hadhi yangu. Nafasi ya Urais ndiyo nayoitaka lakini siwezi kusema ni lini ila jua ipo siku mimi nitagombea nafasi hiyo,” Kala aliiambia Bongo5 muda mchache baada ya kushuka kwenye steji.

Rapa huyo amedai hakuna kitu kinachoshindikana kwenye dunia kama mtu akiamua kufanya jambo lake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents