Siasa
Nakaaya aikacha Chadema,Atinga CCM
Mwanamuziki maarufu wa kizazi kipya nchini Nakaaya Sumari jioni hii ametangaza kukihama chama cha Chadema na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM) Arusha.
Nakaaya Sumari ametangaza hayo jioni hii mbele ya Mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dr. Jakaya Mrisho Kikwete na wana CCM wengine katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha wakati wa mkutano wa kampeni za wilaya ya Arumeru.
Bongo5 iko katika harakati za kumtafuta msanii huyo atuelezee kuhusu kuhamia CCM