Habari
Nakumatt kuzinunua supermarket tatu za Shoprite Tanzania
Wamiliki wa supermarkert za Nakumatt za nchini Kenya wapo kwenye maongezi na wamiliki wa maduka ya Shoprite wa Afrika Kusini kununua maduka matatu ya Shoprite ya nchini Tanzania katika nia yake ya kujipanua zaidi.
Mkurugenzi Mtendaji wa Nakumatt, Atul Shah alisema kampuni hiyo inataka kuzichukua supermarket hizo za Shoprite, ambapo mbili zipo Dar es Salaam na moja jijini Arusha. Kampuni hiyo yenya maduka nchini Kenya, Uganda na Rwanda, tayari inayo supermarket yake mjini Moshi.
Hata hivyo Shah hakuweka wazi thamani ya manunuzi hayo yanayotaliwa kukukamilika miezi mitatu hadi mitano ijayo lakini akasema itawezeshwa kupitia mikopo kutoka kwa taasisi zinazoikopesha kampuni hiyo.
Source: Reuters via ThePost (SA)