Burudani

Nalipwa kwa ajili ya kiki – Gigy Money

Msanii wa muziki Bongo, Gigy Money amesema mara nyingi huwa analipwa ili kufanya kiki.

Gigy ambaye anatamba na ngoma ‘Papa’ amekiambia kipindi cha 5 Selekt, EATV kuwa kutokana na hilo kiki ni kitu ambacho kwake hakitaisha hadi kufa.

“Huwezi amini muda mwingi nalipwa kwa ajili ya kiki, mtu anakulipa kabisa nataka kujulikana anakutia kama ni laki tano mimi nafanya naye. Mimi hazikatakaa kuisha mpaka naingia kaburini, mimi mpaka siku nakufa ni kiki” amesema Gigy Money.

Katika hatua ngingine Gigy Money amesema watu wengi wanaamini pengine yeye ni mwanamke anayejiuza lakini ukweli ni kwamba yeye anapambana na maisha yake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents