Burudani

Nancy Sumari aeleza jinsi alivyojiweka kando na urembo na kujikita na uandishi wa vitabu, aachia kitabu ‘Haki’ (Video)

Miss Tanzania na Miss World Afrika mwaka 2005, Nancy Sumari ambaye kwa sasa amejikita zaidi kwenye uandishi wa vitabu vya watoto amefunguka kukizungumzia kitabu chake kipya cha watoto kiitwacho ‘Haki’ ambacho kimeingia mtaani katika wiki ya Haki za Watoto Duniani.

Nancy ambaye pia ni Mkurugenzi wa Bongo5 na taasisi ya Jenga Hub ambayo inatoa mafunzo ya matumizi ya vifaa vya teknolojia pamoja na ujuzi wa computer programming kwa watoto wa miaka 7 mpaka 12, amesema masuala ya mrembo ameyaweka pembeni kwasasa na kujikita zaidi kutoa elimu kwa watoto kupitia vitabu.

Kitabu hicho ni kitabu chake cha pili kwaajili ya watoto, kwani kitabu kitabu chache cha kwanza ‘Nyota Yako’ kilizinduliwa March 19, 2013.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents