Burudani

Nandy alifikiria kufanya hili baada ya kuvuja kwa video yake ya utupu na Bill Nass

Jambo ambalo ulilifanya kwa siri halafu ghafla ukalikuta tayari limeshawafikiwa watu na kuwa gumzo, unaweza kufanya kitu ambacho hukutarajia tena hata kujitoa uhai.

Hilo lilimkuta Nandy baada ya video yake ya utupu akiwa na Bill Nass ikiwaonyesha katika mahaba mazito ilipovuja mitandaoni na kuteka vichwa vya habari.

Akiongea wenye kipindi cha Leo Tena cha Clouds FM, Nandy amesema kuwa tukio hilo lilimfanya aamani kuacha kabisa muziki na pia hakuona umuhimu wa kuishi lakini baada ya kupata ushauri BASATA kila kitu kilikuwa sawa.

“Nilihisi kukata tamaa kuachana na muziki kabisa sikuona maana ya maisha. Lakini nilipofika BASATA walinipa ushauri na kunihoji binafsi sikuwa na picha mbaya nyuma katika maisha yangu kama kweli nilivujisha picha zile kwa ajili ya Kiki,” amesema msanii huyo.

Hit maker huyo wa Kivuruge ameongeza kwa kusema, “Hali yangu ilikuwa mbaya sana nilipoona ile video sikuamini kabisa macho yangu. Nilizidiwa na Pumu nikakimbizwa hospitali kifupi nilipata Brain Attack niliwaza kuhusu familia yangu nItamtazamaje mama na baba yangu?”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents