Habari

Naomba maombi yenu – Emmanuel Mbasha autaka Ubunge 

Muimbaji maarufu wa nyimbo za Injili Tanzania Emmanuel Mbasha amonyesha nia ya kuutaka Ubunge baada ya leo hii kuchukua fomu ya kugombea katika Jimbo la Iramba Mashariki Wilaya ya Mkalama, Mkoani Singida.

Kutoka upande wa kushoto Emmanuel Mbasha akichukua fomu ya kugombea Ubunge

Akitangaza nia hiyo kwenye picha na ujumbe aliouweka kwenye mtandao wa Instagram Emmanuel Mbasha ameandika kuwa

Mungu kama uishivyo nakuomba nibariki safari yangu hii mpya ya kuwatumikia wananchi wa Mkalama, nimechukua fomu kugombea Ubunge Jimbo la Iramba Mashariki, Wilaya ya Mkalama Mkoa wa Singida, naomba maombi yenu rafiki zangu wote, Mungu ibariki Tanzania

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents