Habari

Nape nakupenda, ulifanya dhambi zako nikakusamehe – Rais Magufuli (+video)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John Magufuli amesema kuwa amemsamehe kwa moyo wote Mbunge wa Mtama Nape Nnauye.

Rais Magufuli amesema hayo akiwa Mtama na kuwaomba wananchi hao, Wampe mbunge huyo ushirikiano wa kutosha ili kuijenga Mtama.

“Najua wananchi wako wanakupenda, Na mimi nakupenda. Ulifanya dhambi zako nikakusamehe. Nape nimeshamsamehe sio mtuhumiwa hana dhambi yoyote naomba mshirikiane nae kuijenga Mtama. ” Rais Magufuli.

Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye mwezi uliopita alikutana na Rais Magufuli Ikulu kwa lengo la kuomba msamaha, Baada ya sauti yake kuvuja mitandaoni akimteta Rais.

Kwa upande mwingine, Rais Magufuli ametangaza kuwa Halmashauri ya Lindi Vijijini ibadilishwe na iitwe Mtama.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents