Burudani
Nas kuachia albamu yake ya 11 mwaka huu
Baada ya kupita miaka mitano tangu ilipotoka albamu ya ‘Life Is Good’ – Nas amepanga kuachia albamu yake mpya mwaka huu.
Rapper huyo amethibitisha kuachia albamu yake hiyo ya 11 wakati alipokuwa akifanya mahojiano na Billboard.
Nas aliulizwa swali, “expect this album before the year is over?” Naye hakusita alijibu kwa kusema, “For sure.”
Albamu nyingine alizowahi kuziachia rapper huyo kutoka mjini New York ni Hip Hop Is Dead, Greatest Hits, Street’s Disciple, God’s Son, Greatest Hits, Untitled na nyingine.