Burudani

Nash MC amjibu Profesa Jay baada ya kuelezewa kama mtu mwenye wivu

Rapper Nash MC amemjibu mkongwe wa muziki wa hip hop nchini Profesa Jay baada ya kumtaja kupitia mtandao wa Twitter kuwa yeye ni kama mmoja wa rappers wanaokejeli harakati za wasanii wa hip hop za kubadilisha ladha ya muziki huo.

Kupitia mtandao huo Nash ameandika:

Mtu mwenye nidhamu ya uoga akiambiwa jambo huona anachukiwa.
Nidhamu ya uoga kwangu ilikaaga upande wa kushoto kitaaaaambo. Upumbavu Ni kipaji cha mtu haijalishi umri. Nna uhuru wa Kuongea nachotaka almuhimu nisivunje sheria za nchi,hakuna pimbi yoyote anaweza kunipangia swali la kuuliza kwenye muziki. Sijui utaenda nchi gani ukute hakuna Hip Hop. Hip Hop aihitaji Kuvuka boda. Ivuke boda iende wapi? Mbinguni? Unaimba kila aina ya muziki ili upate pesa sasa una tofauti gani na Malaya anaetembea na kila bwana apate pesa?? Mwanaume anatakiwa asimamie kila anachokiamini mpaka mwisho. Na ashinde katika imani yake.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents