Michezo
Nasir nje Mwezi Mmoja.
Arsenal imekumbwa na balaa la majeruhi baada ya kuumia goti kwa Samir Nasri ambaye atakua nje ya uwanja kwa muda wa takriban wiki nne.
Kiungo huyo aling’ara kwenye mechi za majaribio za timu hiyo na alifanya kazi kubwa kwenye mechi na Liverpool.Atafanyiwa operesheni ndogo kufuatia kuumia kwake timu hiyo ilipofungana 1-1 na Liverpool juma pili iliyopita.