Shetta amesema anataka kuufanya mtindo wa kucheza muziki alioupa jina Adedede uwe mkubwa kama Shoki wa Nigeria.
Akiongea na 255 ya XXL kupitia Clouds FM, Shetta alisema lengo la kuutumia mchezo huo alioutumia pia Diamond ni kuupa nguvu zaidi.
“Unajua Nigeria kuna Shoki, tunatakiwa kutengeneza style yetu ambayo kila msanii anaweza kuitumia, that’s our plan,” amesema Shetta.
“Usione ajabu ukiona wasanii wengine pia wanaitumia kwasababu tunataka kuitrendisha ile style.”
Amesema watu wanadhani amemuiga Diamond kwasababu ni wagumu kukubali kazi za wengine na kuziendeleza. Hivi karibuni Shetta aliachia video ya wimbo wake ‘Namjua’ ambayo anaonekana akicheza mtindo huo wa Adedede.