BurudaniVideos

Nataka tuifanye Adedede kuwa kubwa kama Shoki – Shetta

Shetta amesema anataka kuufanya mtindo wa kucheza muziki alioupa jina Adedede uwe mkubwa kama Shoki wa Nigeria.

13129821_1681955508724601_1619242928_n

Akiongea na 255 ya XXL kupitia Clouds FM, Shetta alisema lengo la kuutumia mchezo huo alioutumia pia Diamond ni kuupa nguvu zaidi.

“Unajua Nigeria kuna Shoki, tunatakiwa kutengeneza style yetu ambayo kila msanii anaweza kuitumia, that’s our plan,” amesema Shetta.

“Usione ajabu ukiona wasanii wengine pia wanaitumia kwasababu tunataka kuitrendisha ile style.”

Amesema watu wanadhani amemuiga Diamond kwasababu ni wagumu kukubali kazi za wengine na kuziendeleza. Hivi karibuni Shetta aliachia video ya wimbo wake ‘Namjua’ ambayo anaonekana akicheza mtindo huo wa Adedede.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents