Burudani

Naweza kufanya taarab – Timbulo

Msanii wa Bongo Fleva, Timbulo amesema hatosita kufanya muziki wa taarab endapo utakuwa umeliteka soko na muziki wake haupo katika soko.

Muimbaji huyo ameiambia Magic FM ingawa yeye si mpenzi wa taarab na hajawahi kupenda muziki huo ila linapokuja suala la biashara kubadilika ni lazima kwa msanii.

“Naweza kufanya taarabu kwa sababu no way out, kuna kipindi muziki wa taarab ulikuwa unafanya vizuri hata baadhi ya wasanii wengi waliswitch kujaribu kufanya aina ya muziki unaofanana na wa mwambao,” amesema Timbulo na kuongeza.

“Sio nitoe taarab kabisa, ila ni muziki fulani unaofanana na ule wa mwambao ili niweze kusurvive, kwa hiyo ikitokea (taarab) ndio imekua aina pekee ya muziki wenye biashara na muziki wangu sio biashara, nitafanya” amemaliza kwa kusema.

By Peter Akaro

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents