Burudani

Nay aeleza kinachoikwamisha albamu yake na Diamond

Msanii wa muziki wa hip hop, Nay wa Mitego amefunguka kueleza sababu inayochelewesha kutoka kwa albamu yake mpya akiwa na Diamond Platnumz.

Nay wa Mitego na Diamond

Wawili hao waliwahi kushiriki kwenye project ya pamoja ya wimbo ‘Muziki Gani’ ambayo ilifanya vizuri kitaifa na kimataifa.

Akiongea na Bongo5 wiki hii kuhusu ujio wa albamu hiyo, Nay amedai sehemu kubwa ya maandalizi ya ujio wa albamu hiyo yameshafanyika.

“Albamu inakuja kama tulivyowaahidi mashabiki, kuna kazi nyingi zaidi ya hiyo albamu sema muziki ni timing na sasa hivi kila msanii yupo busy na muziki wake. Kwahiyo mimi nadhani muda ukifika albamu itaingia sokoni na niwaambie tu ukweli mashabiki albamu ina nyimbo kali sana,” alisema Nay wa Mitego.

Katika hatua nyingine rapa huyo ambaye anafanya vizuri na wimbo ‘Wapo’ amewataka mashabiki wa muziki wake kukaa mkao wa kula kwaajili ya ujio wa remix ya wimbo huo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents