Burudani

Nay wa Mitego aeleza kwanini alinunua sanamu ya shetani kwa shilingi milioni 5

Nay wa Mitego ni mtu wa maamuzi na mapenzi tofauti na wengine. Ndio maana ukiingia ndani kwake utakutana na sanamu isiyo ya kawaida – ni sanamu ya shetani!

10448990_832778150125234_507563681_n

Rapper huyo ameiambia Bongo5 kuwa sanamu hiyo ni moja ya vitu anavyovipenda zaidi ndani mwake.

“Mimi naipenda na niliinunua hela nyingi tu, ni dola elfu tatu,” amesema Nay.

“Nilitokea tu kuipenda, ni moja kati ya vitu muhimu ninavyovipenda ndani ya nyumba yangu. Kuna sehemu niliinunua sio Tanzania. “Mimi nilitokea kukipenda yaani naipenda sana tena sana na hata ukiingia ndani kwangu utaanza kuiona hiyo,” amesisitiza rapper huyo.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents