Burudani
Nay wa Mitego ana mpango wa kuongeza mtoto wa nne
Nay wa Mitego bado ana hamu ya kuiongeza zaidi familia yake.
Nay wa Mitego akiwa na watoto wake, Munie pamoja na Curtis
Rapper huyo mwenye watoto watatu amesema ana hamu ya kupata mtoto wa nne.
“Suala la uzazi wa mpango nalizingatia sana. Sasa hivi nina watoto watatu bado mmoja tu. Unajua hutakiwi uzae watoto wengi halafu waje kushangaa tu bila msaada,” amesema Nay.
“Mimi hawa wa nne watasoma vizuri kwa sababu tayari toka naanza maisha nilipanga kuja kuwa na watoto wanne.”