Diamond Platnumz
Nay wa Mitego na Diamond waingia tena studio kupika kitu!
Collabo yao, ‘Muziki Gani’ ilikuwa miongoni mwa ngoma zilizotamba zaidi miaka miwili iliyopita, hivyo ukiwaona wameingia tena studio, hakuna shaka kuwa hit nyingine ipo njia.
Nay wa Mitego na Diamond Platnumz wameingia studio kwa mara nyingine kutengeneza wimbo pamoja.
Nay amepost picha akiwa na hitmaker huyo ambaye hivi karibuni alikuwa vekesheni visiwani Zanzibar na mpenzi wake Zari na kuandika:
You know how it is when these two Devils meet…. #Nightsession #BabaKijacho a.k.a #ShabaLanks a.k.a mpya hii.. @diamondplatnumz Kumekuchaaaaaa.”