Habari

Ndalichako aitaka bodi mpya ya TCU kukaza msuli

Waziri wa elimu, sayansi na teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako, ameitaka bodi mpya ya tume ya vyuo vikuu TCU kushughulikia changamoto zilizopo katika tume hiyo baada ya ile iliyokuwepo kuvunjwa.

ndalichako

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa bodi hiyo, Profesa Ndalichako, alisema amekuwa akipokea malalamiko kutoka kwa wanafunzi wa vyuo vikuu kuhusiana na vyuo wanavyosoma hivyo ni wakati wa bodi hiyo kufuatilia kwa ukaribu malalamiko hayo na kuyafanyia kazi.

“Tunaelewa kuwa wanafunzi ni watu wa kulalamika kila wakati, lakini yapo malalamiko ambayo yana tija na ni lazima yatatuliwe,” alisema. “Kwa mfano nilipokea malalamiko kutoka chuo kikuu cha Ifakara mwezi Mei mwaka huu kuhusiana na walimu wa chuo hicho kuvuruga matokeo yao lakini chuo hicho hakijatoa maamuzi yoyote mpaka leo hivyo kuwaacha wanafunzi kubaki nyumbani na kutokujua nini hatma yao,” alieleza Profesa Ndalichako.

Aidha alisema TCU ina mamlaka ya kuvifuatilia vyuo vyote vikuu nchini, pamoja na kufuatilia utendaji kazi wa vyuo hivyo ikiwa unaendana na viwango vilivyowekwa.

BY: EMMY MWAIPOPO

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents