Ndege mpya ya Messi balaa, ngazi zaandikwa majina ya watoto wake, mke na yeye mwenyewe bila kusahau namba 10
Nyota wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi amenunua ndege mpya yenye gharama ya pauni milioni 12 kwaajili ya kutumia katika safari zake akiwa sambamba na familia yake.
Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Argentina ataanza kuitumia ndege hiyo ya kifahari iliyotuwa ikiwa imetimia kila idara kuzunguka ulimwengu akiwa ramstarehe.
Sehemu ya nyuma ya ndege hiyo imechorwa namba 10 ambayo huitumia pindi wapao uwanjani na ufito mweusi unaowakilisha Argentina.
Ngazi za ndege hiyo zikiwa zimeandikwa jina lake, mke wake Antonela pamoja na watoto wake watatu ambao ni Thiago, Ciro na Mateo.
Kwa mujibu wa vyombo mbalimbali vya habari ndege hiyo imekuja ikiwa inaidadiya jumla ya viti 16 ambavyo vinauwezo wa kuvigeuza na kuwa vitanda nane pamoja na vyumba viwili vya bafu sambamba na majiko mawili.
Messi aliingia kipindi cha pili wakati Barcelona ikitoka sare ya goli 1 – 1 dhidi ya Tottenham kwenye mchezo wa michuano ya Champions League hapo jana siku ya Jumanne.