Michezo
Ndemla atua salama Sweden
Klabu ya soka ya Simba imethibitisha kuwa kiungo wake, Said Hamisi Juma Ndemla amewasili salama Sweden tayari kuanza kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa nchini humo.
“Said Ndemla amewasili salama nchini Sweden tayari kuanza majaribio yake katika klabu ya AFC Eskilstima inayoshiriki ligi kuu nchini humo.” Imesema klabu ya Simba.
Safari ya Ndemla Sweden yaota mbawa
Ndemla alipaswa kuondoka Novemba 7 kwenda Sweden kwaajili ya kufanya majaribio katika klabu ya AFC Eskilstuna lakini safari yake ilisogezwa mbele kwa siku mbili hadi tarehe 9 ya mwezi huu.
Simba SC yatoa baraka zote kwa Ndemla kutua Sweden
Ndemla atakuwa huko kwa takribani siku 14 kabla ya kurejea nchini.