Habari
Ndoa ya Janet Jackson na mchumba wake Wissam Al Mana yanukia
Mwanamuziki mkongwe wa nchini Marekani Janet Jackson anatarajia kufungua ndoa na mchumba wake wa Qatar bilionea Wissam Al Mana mwakani. Habari zinadai kuwa wapenzi hao tayari wamechumbiana.
Kwa mujibu wa mtandao wa Us Weekly harusi yao itagharimu mamilioni kwakuwa bilionea huyo amepanga kuwasafirisha ndugu na marafiki zake Janet kwa private jets ili kuhudhuria harusi hiyo nchini Qatar.
Mtandao huo umesema pia kuwa pete ya uchumba aliyovishwa Janet ni kubwa na ya gharama kubwa na mara nyingi amekuwa akiiungua wa kuogopa kuwa ataipoteza.