Burudani

Ndoto ya watanzania kutoa mshindi TPF5 yafutika rasmi


Matarajio ya kupata mshindi kutoka Tanzania katika mashindano ya Tusker Project Fame msimu wa tano jana yamefutika rasmi baada ya mshiriki aliyekuwa amesalia kutoka Tanzania kutoka.

Damiani Innocent Mihayo alifungasha virago jana baada ya jitihada zake za kuonesha kuwa aliingia kwenye probation kwa bahati mbaya kugonga mwamba. “Damian is Good…Bad choice ya nyimbo aliyoimba,he also lacks star quality,” aliandika mfuatiliaji mmoja wa mashindano hayo.

“Huyu jamaa (Damian) like two weeks ago alichemka mistari ya Ali Kiba, shame! Aaaa project fame alikua Lina, Msechu na kidoooogo Aneth, yaani hata Hemedi namsifu, he knew how to play the game. Ndo makosa tunafanya hata BBA. Watu kama Hemedi au hata Wema ni watu wanajua kucheza na ni rahisi watanzania kutoa support. Hilda na Julio ppphhheeeew,” aliandika mwingine aitwaye Yvonne kupitia Facebook.

Kutokana na kutolewa kwa Damian sasa watanzania watabakia kuwashuhudia tu washiriki kutoka Uganda, Kenya, Sudan Kusini, Rwanda na Burundi katika shindano hilo. Katika hatua nyingine wiki hii Universal Music Group (UMG) imeingia mkataba na shindano hilo ambapo itamsimamia mshindi wa mwaka huu. Pia itasimamia kurekodi albam ya pamoja ya washiriki kumi bora wa mwaka huu.

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents