Michezo
Ndoto za Johanna Konta za zimwa China
Mchezaji tenis raia wa Uingereza mwana dada, Johanna Konta ameshindwa kutamba katika michuano ya wazi ya Wuhan nchini China baada ya kukubali kipigo kutoka kwa Ashleigh Barty katika mchezo wa raundi ya pili ya michuano hiyo ambayo aliamini angefanya vizuri.
Mchezaji tenis raia wa Uingereza mwana dada, Johanna Konta
Konta mwenye umri wa miaka 26, amekubali kipigo cha jumla ya seti 6-0 4-6 7-6 (7-3) kutoka kwa mwana dada mwenzake raia wa Australia, Ashleigh Barty.
Mchezaji tenis raia wa Australia, Ashleigh Barty
Katika michuano hiyo mwana dada raia wa China, Naye Peng Shuai ameibuka kidedede kwa jumla ya seti 7-6 (9-7) 6-7 (5-7) 7-6 (7-3) baada ya kumshinda, Petra Kvitova kutoka Jamhuri ya Czech.