Burudani
Ne-Yo na mchumba wake mjamzito Crystal Renay kufunga ndoa mwezi ujao
Mwimbaji wa RnB kutoka Marekani, Ne-Yo na mchumba wake wanatarajia kufunga pingu za maisha mwezi ujao.
Ne-Yo na mchumba wake wa muda mrefu Crystal Renay ambaye ni mjamzito hawajatangaza rasmi tarehe ya kufunga ndoa, lakini kwa mujibu wa mtu ambaye ni miongoni mwa waalikwa aliyevujisha mtandaoni kadi ya mwaliko inaonesha ndoa itafungwa February 20, 2016.
Mwezi September 2015, Ne-Yo alikanusha vuvumi ulioenea kuwa tayari walikuwa wamefunga ndoa, lakini akakiri kuwa mchumba wake ni mjamzito na kuahidi kufunga ndoa mwaka huu 2016.
Clearing the air..@mscrystalrenay and I are ENGAGED to be married next year. And yes we are expecting. #FromTheHorsesMouth
— NE-YO (@NeYoCompound) August 31, 2015