Habari

New Music: Stamina ft Jux – Alisema


Stamina ameachia ngoma mpya iitwayo Alisema ft Jux leo tarehe 1/3/2012 kama dedication kwa Mama yake ambaye alifariki tarehe kama ya leo, may her soul rest in peace.

Studio: Snap Records – Producer: Kevy – Songwriter: Stamina & Jux

Lyrics:

Intro: Is moro town beib, You know what kevy? this is so conscious men

Vers 1: Stamina
Sio kila mchaga muuza duka,so nisiogope kuitwa mangi
Kupanda na kushuka,ndio chart isiyohitaji rangi
Bora kuitwa mshamba,kwenye group la matapeli
Subira ikikosa kamba,nijipange kuivuta heri
Alisema nisilete uchizi,mbele ya daktari wa akili
Nisiwe na hasira za mkizi,ili mvuvi anifanye dili
Kukosa na kupata,ndio mechi isiyokua na draw
Kama maisha karata,mchangaji nimkabe koo{ooooh}
Madawa ya kulevya,niogope yatanipa uchizi
Maishani nisiwe dereva,kwenye basi la wazinzi
Kengeza ndo macho yangu,nisimcheke mwenye chongo
Nipendezeshe maisha yangu,kama dressing table ya mkongo
Nisile ada kisa demu,mapenzi hayana mradi
Maisha ni ps game, hayachezeki bila pad
Elimu ya mtaani,niijue ili nikuze ukoo
Ila elimu ya darasani,nisihitimu bila ya joh{alisema}

Chorus: Jux
Nifanye nachofanya bwana mimi nisizubae,uwezo ninao{alisema}
Maneno yakisemwa wala mimi nisishangae,niachane nayo{alisema}
Ubinadamu kazi{alisema},nisiwe na haraka na maisha{alisema}
Nisichague kazi{alisema}nakumbuka ieeeiiiiiiii

Vers 2: Stamina
Usoni nisipretend ugumu,wakati moyoni nina usharo
Ugangstar sio kuvuta ndumu,nijipange nitafuta mipalo
Kama pesa hazilali,mtafutaji nisichonge kitanda
Asali ikiwa juu ya dali,mlinaji nisichome kibanda

Alisema mjini mipango,sio urefu wa magorofa
Samaki akiliwa na chambo,nijue mvuvi ameshaanza urofa
Nisinywe gongo na biskuti,nikadhani ndio janja ya teja
Nikaze buti ili nijibust,wapinzani wasiniite kinega
Kama muda ni pesa,nifungue account ya saa
Nisiseme boom linatesa,huku principle anashinda bar
Maisha trailer za kanumba,nisiogope kufa kiuongo
Mimba ya ujinga haina mkunga,nitafute ujanja kwa usongo
Nisimdharau fukara,kisa nimemzidi kipato
Mtoto nisimfanyie tohara,akikua aniite pilato
Fisadi akiwa jogoo,tetea nitafute kambi
Mziki una kwashiorkor,nisiache hadi unipe kitambi{alisema}

Chorus: Jux
Nifanye nachofanya bwana mimi nisizubae,uwezo ninao{alisema}
Maneno yakisemwa wala mimi nisishangae,niachane nayo{alisema}
Ubinadamu kazi{alisema},nisiwe na haraka na maisha{alisema}
Nisichague kazi{alisema}nakumbuka ieeeiiiiiiii

Vers 3: Stamina
Nisishangae kukuta bwanga,kwenye chumba cha mamodel
Ila nishangae kuziona shanga,kwenye kiuno cha mtoto mdogo
Kipimo cha utapeli,hakipimwi na mzani wa ubongo
Nisibishane na ukweli,ikiwa nina chembe za uongo
Mfupi ndio aliyegundua ngazi,ilimradi apate virefu
Nisimtukane mzazi,nitapata radhi ya ukosefu
Selemara arudi veta,mende akiangusha kabati
Na daudi akipigwa ngeta,nijue kesi kwa goliati
Primary na shule ya msingi,zina utofauti wa kimasilahi
Inabidi nione vifo vingi,ili nijue thamani ya uhai
Nguvu za uongo wa video,zisinipotezee ujana
Nisijiite jembe huku kimeo,wakati pabichi nakwama
Nikikosa fasta nitubu,masizi yasigeuke kiwi
Na nisiogope kuitwa bubu,kwenye kundi la viziwi
Nis Chorus iforce penzi kwa changu,ni bora nikatumia detto
Na moro ndio mkoa wangu,nikiukana wataniita petro{alisema}

Jux
Nifanye nachofanya bwana mimi nisizubae,uwezo ninao{alisema}
Maneno yakisemwa wala mimi nisishangae,niachane nayo{alisema}
Ubinadamu kazi{alisema},nisiwe na haraka na maisha{alisema}
Nisichague kazi{alisema}nakumbuka ieeeiiiiiiii

Bridge: Jux
Uwezo ninao{alisema}
Niachane nao{alisema}

Outro: Stamina
Kama Mungu alitoa,tusishangae anapo twaa
Amini kila binadamu alizaliwa shujaa
So this one,is dedicated to all who lost their beloved ones

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents