Michezo
Newcastle ya mtimua kocha wake Steve McClaren
Klabu ya Uingereza ya Newcastle imemtimua rasmi kocha wake Steve McClaren.
Kocha huyo alishinda mechi sita kati ya 28 katika kilabu hiyo ambayo inakaribia kushushwa daraja katika ligi hiyo.
McClaren na timu yake walizomewa baada ya kushindwa 3-1 na kilabu ya Bournemouth katika uwanja wa nyumbani wa St James Park ikiwa ni mara yao ya tatu kushindwa.
Aliyekuwa kocha wa Liverpool,Chelsea,Real Madrid na Intermilan, Rafael Benitez huenda akachukua mahala pake.
McClaren alitia saini kandarasi ya miaka mitatu na Newcastle mnamo mwezi Juni baada ya kilabu hiyo kuzuia kushushwa daraja katika siku ya mwisho msimu uliopita