Michezo
Neymar na Baba ake kwenye kesi ya ukwepaji Kodi
Mchezaji wa Barcelona pamoja na timu ya taifa Brazil Neymar Jr pamoja na baba yake wameamriwa na mahakama huko Brazil kulipa kiasi cha Euro 100,000 sawa na milioni 200 za Kitanzania kama faini baada ya kushindwa kulipa kodi.
Mwanasheria wa mchezaji huyo amesema Neymar hajaridhishwa na dhabu hiyo na anatarajiwa kukata rufaa.
Neymar na baba yake wanakabiliwa na faini hiyo iliyotokana na kodi ya mapato tangu mwaka 2012.
Neymar pia ametajwa kwenye kesi inayoendelea kufanyiwa uchunguzi ya ukwepaji kodi kwenye uhamisho wake kutoka Santos kwenda Barca – kodi inayodaiwa kwenye dili hilo inafikia 13 million euros.