Patrick Nyanzi aka Pato pamoja naye Eddie Mpagi almaarufu kama Ayde E kwa pamoja wanaunda kundi la Ngoni lenye maskani huko Kampala, Uganda. |
Story by: Daniel Nyalusi
Patrick Nyanzi aka Pato pamoja naye Eddie Mpagi almaarufu kama Ayde E kwa pamoja wanaunda kundi la Ngoni lenye maskani huko Kampala, Uganda.
Nyimbo yao ya kwanza kabisa ambayo nayo ilikuwa na mahadhi ya RnB “Sekiriba Kya ttaka” ilitoka 1998.
Kundi hilo ambalo linaimarika kadri siku zinavyokwenda limejipatia umaarufu katika siku za karibuni na nyimbo zake za DiGi na NASIIMA GWE ikimaanisha “Tuko Pamoja”.
Wasanii hao wanatumia staili ya muziki wake kama Good Swing (Afro Pop) ambayo inachanganya R n’ B na mirindimo ya Kiafrika kwa kutumia mtindo wa Zouk.
Ngoni wanatarajiwa kuja kutumbuiza jijini Dar es Salaam tarehe 16 ya mwezi huu katika show ambayo itaongozwa nae Gwiji linalo ongoza kwa mauzo kwa wasanii wa Kiafrika nchini Marekani AKON, Ngoni wameshafanya maonesho katika miji mbali mbali Afrika na Ulaya ikiwemo Sweden na Rwanda.
Source: Bongo5