Uncategorized
Ngorongoro Heroes yafungwa na Nigeria
TIMU ya soka ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 20, Ngorongoro Heroes jana imeanza vibaya kampeni za kuwania kucheza Fainali za Afrika kwa vijana wenye umri huo, zitakazofanyika nchini Algeria mwakani, baada ya kufungwa na Nigeria mabao 2-1 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Wachezaji wa Ngorongoro wamesema kwamba uwezo wa kuwafunga Nigeria 2-0 wiki ijayo nchini kwao ili kusonga mbele kwenye Fainali za Afrika upo, iwapo watafanyia vema makosa yao.