Michezo
Nguvu ya Soda? Ryan Giggs auanza vyema umeneja wa Man United kwa timu yake kuichapa Norwich 4-0
Kete ya kwanza ya Ryan Giggs kama meneja wa muda wa Manchester United imeanza vyema usiku wa Jumamosi kwa mashetani wekunda kuichapa kichapo cha mwezi Norwich.
Kocha wa muda wa Man United, Ryan Giggs
Wayne Rooney na Juan Mata wamefunga magoli mawili kila mmoja kwenye mechi hiyo ya Old Trafford.
Giggs aliteuliwa kuwa kocha wa muda wa timu hiyo baada ya David Moyes, kutimuliwa.