Burudani

Ni kushoot video mpya au bata tu? Alikiba atinga Tarangire (Picha)

Alikiba na timu yake kutoka label ya Rockstar4000 wameitembelea mbuga ya wanyama ya sita kwa ukubwa nchini ya Tarangire, iliyopo mkoani Manyara.

11008153_851190041594555_1638435709_n
Alikiba akichukua picha kwenye mbuga ya wanyama ya Tarangire

Muimbaji huyo wa ‘Mwana’ aliyekuwa miongoni mwa wasanii waliotumbuiza kwenye tamasha la Sauti za Busara mwaka huu, amepost picha kadhaa akijiachia kwenye viota vya starehe vilivyopo kwenye mbuga hiyo ikiwa na pamoja na selfie kadhaa na wanyama.

924766_506961229442886_1578967291_n
Alikiba akiwa na timu yake akiwemo Director of Talent and Music Pan Africa – Rockstar 4000 / Sony Music Africa, Seven Mosha kushoto kwake

Haijulikani iwapo ameenda kutalii tu au kuna kazi inaendelea huko lakini picha zake amekuwa akiziambatanisha na hashtag #chekechacheketua ikiashiria kitu kipya kutoka kwake.

11008089_653791714747238_1459410551_n
Selfie na tembo926261_867406193324315_400867330_n
Bata Batani

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents