Picha

Ni kweli Keri Hilson aliidiss Afrika kwa kutuita starving Africans?

Huenda Keri Hilson akaja Tanzania na Kenya katikati ya mwezi ujao (December) akiwa tayari amewakera waafrika kwa tweet yake ambayo yeye anasema hakuiandika. Tweet hiyo inayotuponda waafrika kuwa tunakufa na njaa.

Katika tweet hiyo Keri aliandika, “IT’S THANKSGIVING ! Just did that 19 hour flight back from Ghana and most definitely am going to eat like a pig for the starving Africans.”

Tweet hiyo iliamsha hasira kubwa wa waafrika waliochukizwa na kitendo cha msanii huyo kulidharau bara la Afrika kiasi hicho.

Jana imemlazimu msanii huyo kukanusha kuandika tweet hiyo kwa madai kuwa kuna mtu aliitengeneza kwa kutumia program ya photoshop ili kumkosanisha na waafrika.

“Wow. People actually believe I’d say that? I woke up & saw a fake photoshopped tweet abt me dissing Africa?! C’mon man. Really? Disgusting.

“REALLY didn’t wanna spend any part of my day combating foolishness 🙁 But I simply cannot hv u doubting my sincerity abt my love for Africa!”

“And for those still skeptical, I wasn’t even in Ghana this trip. They didn’t even have the facts right to make it believable.”

Tumwamini nani?

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents